MLM Gateway - Helping network marketers build their business

Ghasia Afghanistan: Mwanamke anayenyonyesha waliofiwa na mama zao kwa shambulio


"Nilikuwa namnyonyesha mtoto wangu kisha nikaanza kufikiria wengine na kuhuzunika sana. Niliona vile wale watoto wengine wanavyotaabika," amesema Firooza Omar.

Jumanne wiki hii, watu karibia 24 ikiwemo watoto wachanga, kina mama na wauguzi waliuawa kinyama kufuatia shambulio lililotekelezwa na wanamgambo katika chumba cha kujifungua kina mama nchini Afghanistan mjini Kabul.

Firooza, 27, alisikia kuhusu shambulio hilo kupitia televisheni. Alielewa ukubwa wa tatizo lililopo baada ya kuzungumza na rafiki yake na kuona picha mbaya za shambulio zilizokuwa kwenye mitandao ya kijamii.

Yeye mwenye ni mama wa mtoto mvulana wa miezi minne.


Firooza Omar with her four-month-old boy.
Firooza alipata mtoto wa kiume hivi karibuni

Wakati anamnyonyesha mtoto wake, alijiwa na fikra za watoto wengine walioachwa mayatima.


Utu na ujasiri

Ameamua kwenda kusaidia watoto wengine wachanga waliopoteza mama zao katika shambulio hilo.

Kilichofuata ni kuonesha ukarimu wake na ujasiri alio nao.


A woman sits next to new-born babies who lost their mothers following a suicide attack on a maternity hospital in Afghanistan
Baadhi ya watoto hawakuwa na wakuwahudumia baada ya mama zao kuuawa kwa shambulio la wanamgambo mjini Kabul

"Wakati ulipokuwa unawadiwa wa kufungua baada ya kufunga, (shambulio hilo limetekelezwa wakati wa Ramadhani, mwezi mtukufu wa Kiislamu), nilimwambia mume wangu kuhusu nia yangu ya kusaidia watoto ambao wamekuwa mayatima."

Mume wake alimkubalia moja kwa moja na kumuhakikishia kwamba atakuwa anamuangalia kijana wao nyumbani.

Wakati huo Vikosi Maalum vya Afghan vilinusuru kina mama na watoto 100 katika hospitali ya Dasht-e-Barchi na idadi kubwa ya watoto wachanga wakapelekwa katika hospitali ya watoto ya Ataturk takribani kilomita 2 kutoka pale anapoishi Firooza.

Watoto wakili

Umbali aliotembea kwa gari huenda ulikuwa mfupi zaidi lakini wenye kuhatarisha maisha yake katika mji ulioghadhabishwa, kushtuma na kuingiwa na hofu baada ya kutokea kwa shambulio.

Firooza Omar in front of a cupboard holding books
Firooza anasema mume wake amemuunga mkono kwa asilimia 100 azimio lake la kunyonyesha waliofiwa na mama zao

"Nilipokwenda hospitalini, niliona watoto karibia 20. Baadhi yao walikuwa wamejeruhiwa. Nilizungumza na wauguzi na wakaniambia kwamba ninyonyesha watoto wanaolia sana."

Kisha akanyonyesa watoto wanne, mmoja baada ya mwengine.

Kabla ya Firooza kuwasili, wauguzi walikuwa wanajaribu kuwapa chakula kilichotengenezwa kwa maziwa ya unga.

"Baadhi ya watoto walikuwa wanakataa kunywa maziwa hayo." Firooza anakumbuka.

Kutuliza watoto waliokuwa wanalia hospitali

Aliwapa watoto hao matumaini ya kuendelea kuishi.


Firooza Omar. speaking at a seminar
Firooza anasema kingo cha ghasia zinazotokea Kabul zinafadhaisha raia kama yeye

"Nilipowanyonyesha walitulia. Nilifurahi kuweza kuwasaidia."

Baada ya kurejea nyumbani, ilikuwa ni zamu ya kijana wake kunyonya.

"Baada ya saa mbili, nilimnyonyesha mtoto wangu wa kiume." Firooza anasema.

Aliandika kuhusu tajriba hiyo aliopata kwenye mtandao wa kijamii na kusihi kina mama wengine kwenda kwenye hospitali hiyo kusaidia kunyamazisha watoto wengine waliokuwa wanalia


Anasema baadhi ya wanawake wamejitokeza na kunyonyesha watoto hao.

Baada ya usiku wa shambulio, Firooza pia amefanikiwa kutembela hospitali hiyo siku mbili zilizofuata.

Anasema hilo limewezekana kwasababu mume wake anamuunga mkono na kumsihi kufanya hivyo.

'Uhalifu wa kivita'

Hadi kufikia sasa hakuna ambaye amedai kuhusika na shambulio hilo lililotokea Jumanne, ambalo limeelezewa na makundi ya kutetea Haki za Binadamu kama 'uhalifu wa kivita'.

Serikali ya Kabul imeagiza jeshi kutafuta waliotekeleza shambulio hilo.


Mourners carry a covered dead body during a burial ceremony at a cemetery in Kabul, Afghanistan
Kwa kuzingatia tamaduni za dini ya Kiislamu, waathirika wamezikwa siku moja baada ya shambulio

Aidha, mji wa Kabul umekuwa ukishuhudia ghasia katika kipindi cha miongo minne iliyopita ya vita na migogoro.

Vifo vilivyotokea wiki hii kwa kina mama na watoto wachanga kutakumbukwa kama moja ya matukio mabaya zaidi kuwahi kutokea duniani.

Firooza anasema amefadhaishwa na ghasia zisizoisha ambazo zimekuwa zikishuhudiwa katika mji wake wa nyumbani.

"Badala ya kushikiliwa na watoto wao, watoto hawa wako hospitali, wakinyonyeshwa na watu wasiowajua." anasema.

Kama daktari wa magonjwa ya akili, Firooza anataka kuchangia pakubwa katika kuhakikisha raia wengi wa Afghan wanapona majera na machungu ambayo wamekuwa wakikabiliana nayo.

'Ninafuraha kulelea mtoto'

Amewasiliana na baadhi ya rafiki zake kutafuta pesa za kununua nepi na maziwa ya unga, kwa ajili ya watoto hao wakati ambapo hawatakuwa tayari kunyonya.


Firooza Omar speaking at a conference
Firooza anafikiria kuasili mtoto aliyeachwa bila familia kwasababu ya shambulio hilo

Anasema, mbali na wale waliojeruhiwa, watoto wengine kwa sasa wanaruhusiwa kuondoka hospitali ya watoto ya Ataturk.

Lakini anawasiwasi kuhusu wale ambao hawana familia na kujiuliza wataenda wapi?

Kipaumbele itakuwa ni kwa watoto mayatima." Alisema, kwa uhakika.

"Nitakuwa mwenye furaha ikiwa nitaweza kuchukua mtoto na kumlea pamoja na kijana wangu."


Share:

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Kumbukumbu la Blogu

MAARUFU

ZA HIVI KARIBUNI