MLM Gateway - Helping network marketers build their business
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo BURUDANI. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo BURUDANI. Onyesha machapisho yote

TANZIA: Babu Njenje afariki dunia


mwanamuziki mkongwe wa Bendi ya Kilimanjaro maarufu kama Wana-Njenje, Mabrouk Hamis Omar almaarufu kama Babu Njenje amefariki dunia leo jijini Dar baada ya kuugua kwa muda mrefu.










Marehemu Babu Njenje ambaye alizaliwa mwaka 1947 Wilayani Pangani, Tanga,alianza kazi ya Muziki wakati anasoma shule ya Usagara Sekondari Mkoani Tanga, na baadaye akajiunga na Band ya Love Burg huko Tanga, kisha Marehemu alijunga na Band ya Revolution na ilipofika mwaka 1989 yeye pamoja na wanamuziki wenzake akiwemo Abdallah Dulla,Hemed Salim Chuki, Babu Njenje, Mohamed Mrisho, Waziri Ally pamoja Keppy Kiombile walianzisha The Kilimanjaro Band.


Share:

Diamond Platnumz ,WCB watoa wimbo wa pamoja ‘Quarantine’






Lebo ya muziki wa Bongo Fleva WCB Wasafi imeungana na kutoa wimbo mmoja wa  ‘Quarantine’ ambapo wamo Diamond Platnumz, Rayvanny, Mbosso, Lavalava, Zuchu na Queen darlin.






https://youtu.be/wwf09xtoQHU

Share:

“Hakuna Beef Na Lady Jaydee”- Meneja wa Ally Kiba


Meneja wa msanii wa Bongo Fleva Ali kiba ameweka wazi kuwa hakuna ugomvi wowote baina ya msaani huyo na Lady Jaydee





Kauli ya meneja huyo inakuja kutokana na majibu ya Lady Jaydee alipoulizwa na shabiki mmoja kwenye mtandao wa twitter iwapo itafanya collabo na Ally Kiba





“Jay dee ni msaanii tunaye mheshimu ni dada na sidhani kama kuna ugomvi wowote baina yake yeye na Kiba maan tumeshirikiana mara nyingi kipindi akiwa Rockstar (label ya Ali kiba) labda kama kuna shida nyingine ila sisi hatuna shida” amesema Aidan Charlie alipoulizwa na clouds Tv





Ikumbukwe kuwa mara ya mwisho Ally Kiba kushirikiana ilikuwa mwaka 2012 walipotoa wimbo wa Single Boy wa Ali Kiba, Jay Dee alipoulizwa kama atafanya collabo na mkali huyo alisema hana mpango na afikirii leo wala kesho


Share:

Gloomy Sunday, Wimbo Uliosababisha Watu zaidi ya 100 Kujiua


Gloomy Sunday (Jumapili ya Huzuni) ni wimbo uliotungwa na Rezso Seress (Rudi Spitzer), msanii kutoka nchini Hungary mwaka 1933. Reszo alitunga maneno ya wimbo huo na kupiga mwenyewe ala ya huzuni ya wimbo huo, baada ya kuachwa na mpenzi wake.





Inaelezwa kwamba kitendo cha kuachwa na mwanamke aliyekuwa akimpenda sana, kilimfanya apatwe na huzuni kali na msongo wa mawazo, na katika kipindi hicho ndipo alipopata wazo la kutunga mashairi na baadaye kuutengeneza wimbo huo.





Kwa sababu aliuimba akiwa na huzuni kali, wimbo nao ulijawa na hisia kali, za mtu anayelalamika kuvunjwa moyo na mpenzi wake, akifananisha kitendo cha kuachwa kuwa sawa na kufiwa na mpenzi aliyekuwa anampenda.





Awali ulionekana kuwa wimbo wa kawaida wa huzuni, lakini matukio ya watu kuyakatisha maisha yao baada ya kuusikiliza mara nyingi wimbo huo kwa kuurudiarudia yalianza kuripotiwa, wengine wakiacha kabisa ujumbe kwamba wamejiua baada ya kusikiliza wimbo huo.





Miaka miwili baadaye, serikali ya Hungary iliupiga marufuku wimbo huo, hata hivyo tayari ulikuwa umesambaa sana, kiasi kwamba watu bado waliendelea kuusikiliza, hasa pale inapotokea mtu ameachwa au ameumizwa na ampendaye.





Sifa za wimbo huo zilianza kusambaa duniani kote na mwaka 1936, wanamuziki wa Marekani na Uingereza waliutafsiri wimbo huo kwa lugha ya Kiingereza, kutoka lugha ya awali ya Ki-hungary, bado tatizo lilelile likawa linaendelea hata kwa matoleo yaliyotafsiriwa, watu wakawa wanaendelea kujiua baada ya kuusikiliza.





Mwanzoni mwa miaka ya 1940, toleo la Kiingereza la wimbo huo lilipigwa marufuku nchini Uingereza baada ya idadi ya waliokuwa wakijiua kuzidi kuongezeka lakini Marekani na sehemu nyingine duniani wimbo huo uliendelea kupigwa





Miaka michache baada ya wimbo huo kumpatia mafanikio makubwa na kuwa gumzo dunia nzima, Seress aliamua kumtafuta mwanamke aliyemuacha na kusababisha atunge wimbo huo, lengo lake likiwa ni kujaribu kumbembeleza ili warudiane kwani kama ni pesa, tayari alikuwa nazo baada ya wimbo huo kuwa maarufu dunia nzima.





Hata hivyo, katika hali ya kustaajabisha, inaelezwa kwamba Seress alipofika mahali alipokuwa akiishi mwanamke huyo, alikuta watu wamejaa, baadaye ikabainika kwamba mwanamke huyo amekunywa sumu na kujiua na kwenye chumba alichojiulia, ilibainika kwamba alikuwa akisikiliza wimbo huo na pia aliacha ujumbe wenye maneno mawili, kama sababu za kujiua kwake; Gloomy Sunday.





Inaelezwa kwamba Seress alibaki na hatia kubwa ndani ya moyo wake, akiamini kwamba yeye ndiyo chanzo cha kifo cha mwanamke huyo na mwaka 1968, naye aliamua kuyakatisha maisha yake kwa kujirusha ghorofani kupitia dirisha la chumba alichokuwa akiishi, nchini Budapest.





Seress aliacha ujumbe kwamba ameamua kuyakatisha maisha yake baada ya kuona wimbo alioutunga, umekuwa sababu za watu wengi kujiua hivyo anahisi hatia kubwa ndan ya moto wake, akawaomba radhi ndugu na marafiki wa wote waliojiua kwa sababu ya kusikiliza wimbo huo.





Lyrics (Literal Translation)
On a sad Sunday with a hundred white flowers
I was waiting for you, my dear, with a church prayer
That dream-chasing Sunday morning
The chariot of my sadness returned without you.
Ever since then, Sundays are always sad
Tears are my drink, and sorrow is my bread.
Sad Sunday. Last Sunday, my dear, please come along,
There will even be priest, coffin, catafalque, hearse-cloth.
Even then flowers will be awaiting you, flowers and coffin.
Under blossoming (flowering in Hungarian) trees
My journey shall be the last.
My eyes will be open, so that I can see you one more time
Do not be afraid of my eyes as I am blessing you even in my death.
Last Sunday."


Share:

ZA HIVI KARIBUNI