Idadi ya waliofariki kutokana na ghasia ambazo zinaendelea nchini Afrika ya kusini imefikia 212,kutoka vile 117 vilivyoripotiwa hap awali.
Waziri wa nchi,ofisi ya rais nchini umo,Khumbudzo Ntshavheni amesema kwamba vifo vilivyoongezeka vimetokea jimbo la kwa zulu-natal,ambapo ndipo kwenye kiini cha machafuko hayo kwa sasa.
Hadi sasa watu zaidi ya 2,500 wameshakamatwa kutokana na vurugu hizo zilizokaa karibu wiki nzima,zikiambatana na uchomaji wa majumba ya biashara na uporaji.
Rais wa Afrika kusini Cyril Ramaphosa ameahidi kuwafatilia wale waliopanga njama ili kuanzisha vurugu hizo. Kwa sasa utulivu umeanza kurejea nchini humo.
hii ni hatari sana
JibuFuta