MLM Gateway - Helping network marketers build their business

Benki ya biashara Tanzania (TCB) yafunguliwa rasmi

Waziri wa fedha na mipango,mheshimiwa Mwigulu Nchemba amefungua rasmi benki ya Taifa ya biashara (TCB),ambayo ni muunganiko wa benki mbili nchini, TIB na TPB ikiwa na shabaha ya kuundwa kwa benki kuu ya biashara ya serikali yenye ushindani katika soko ikitoa huduma za kibenki na biashara.

Akitoa maelezo hayo wakati wa uzindizi wa benki hiyo,waziri huyo amesema kwamba benki hizo zimeunganishwa kisheria,hivyo wafanyakazi wa benki hiyo wanapaswa kujituma na kuwa na ubunifu katika kutimiza majukumu yao ya kikazi sambamba na kuenda na malengo na maono ya benki hiyo.

Pia waziri huyo ameongeza kwa kusema kuwa wateja wote waliokuwa katika benki mbili za mwanzo wataendelea kuhudumiwa na benki hiyo ya TCB kwa uweledi wa halii ya juu.

Mwisho waziri Mwigulu nchemba amewaasa taasisi za mabenki kupaunguza riba kwa wateja wao,ikiwa pamoja na kuangalia jinsi wanavyofilisi mali za wateja wao,pindi wanaposhindwa kurudisha mikopo yao.


Share:

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MAARUFU

ZA HIVI KARIBUNI