MLM Gateway - Helping network marketers build their business

Mbunge aitaka serikali kuzungumzia ‘vifo vitokanavyo na ugonjwa wa kupumua’

Mbunge wa jimbo la Mbulu nchini Tanzania ameelezea wasiwasi wake kuhusu vifo vinavyotokana na ugonjwa wa kupumua vinavyotokea kwa wingi katika jimbo lake, Gazeti la Mwananchi limeripoti.

Katika kikao cha bunge mjini Dodoma, bwana Zacharia Isaay ameitaka Serikali ya Tanzania kueleza kina sababu inayopelekea watu kufa kwa ugonjwa unaofanana, ambao huwa wanaita 'pneumonia', matatizo ya kupumua

"Serikali iache kigugumizi jimboni kwangu watu wanakwisha Spika,"amesema Isaay.

Mbunge huyo ameelezea wasiwasi wake katika msimu huu wa baridi jimboni labda hali inaweza kuwa mbaya zaidi.

"Jana nilikwenda hospitali ya hapa Benjamin Mkapa (Dodoma) kwa ajili ya kufanya vipimo lakini wakaniambia mitungi ya gesi imejaa,watu ni wengi sasa nimesema kama watu watanichukia basi lakini nimesema," Mwananchi imemnukuu mbunge huyo.

Aidha, Mbunge huyo ameomba Serikali kuangalia namna ya kuboresha dawa za miti shamba ambazo ameeleza kuwa zinasaidia kwa kiasi kikubwa lakini akabainisha kuwa zinapatikana kwa gharama kubwa.


Share:

China yazima matangazo ya BBC baada ya UK kuipiga marufuku CGTN

Mamlaka ya utangazaji ya China imelipiga marufuku shirika la utangazaji la Uingereza BBC kurusha matangazo yake nchini humo, ikilituhumu kwa kukiuka miongozi, kufuatia ripoti yenye utata kuhusu nama nchi hiyo inavyowatendea watu wa jamii ya wachache ya Uinghur. Uamuzi huo umekuja siku chache tu baada ya mamlaka ya mawasiliano ya Uingereza kufuta leseni ya shirika la utangazaji la CGTN kwa kukiuka sheria ya Uingereza kuhusu umiliki unaoungwa mkono na serikali, na kusababisha shutuma za hasira kutoka London. Hatua hiyo inazidi kuyaweka pabaya mahusiano katika nchi hizo mbili, ambayo yametiwa doa na hatua ya China kuanzisha sheria ya ya usalama katika koloni la zamani la Uingereza la Hong Kong. Uingereza pia imelipiga marufuku shirika la teknolojia ya mawasiliano la China Huawei kutoshiriki katika mfumo wa mawasiliano wa G5, baada ya Marekani kuelezea wasiwasi kwamba shirika hilo linatumiwa na serikali ya China kuzifanyia uchunguzi nchi nyingine. Katika tangazo la usiku, mamlaka ya usimamizi wa redio na Televisheni ya China (NRTA), imesema report za BBC World News kuhusu China zilibainika kukiuka vibaya miongozo ya utangazaji.


Share: