MLM Gateway - Helping network marketers build their business

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo March 31, 2021






Ni siku nyingine njema, kutoka Dar es salaam leo March 31, 2021,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za nyuma za Magazeti ya Tanzania.


















































































Share:

Kampuni ya Nike yawasilisha kesi kwa madai ya kuhusishwa na Viatu vyashetani






Satan Shoes




Kampuni ya Nike inashitaki ubunifu wa kampuni ya MSCHF iliyopo Brooklyn juu ya uzinduzi wa kile kinachosemekana kuwa "Kiatu cha shetani" chenye tone la damu ya kweli ya binadamu kwenye soli za viatu.





Viatu hivyo vinavyouzwa kwa dola 1,018 sawa na (pauni 740), ambavyo vimechorwa alama ya msalaba iliyopinduliwa na pentagramu (nyota ya ncha tano katika duara) na maneno "Luka 10:18", vimetengenezwa kwa kuboresha muundo wa kiatu cha Nike Air Max 97s.





Kampuni ya MSCHF ilitoa jozi ya viatu 666 Jumatatu ikishirikiana na mwanamuziki Lil Nas X na kusema kwamba vyote viliuzwa chini ya dakika moja.





Kampuni ya Nike imedai kuingiliwa kwa chapa au alama ya biashara ya kampuni yake.





Viatu vya rangi nyeusi na nyekundu "vilivyotolewa" na kampuni ya MSCHF Jumatatu, kulikwenda sambamba na uzinduzi wa nyimbo mpya ya mwanamuzi Lil Nas X ya Montero ya (Call Me By Your Name), ambayo ilitolewa kwa mara ya kwanza kwenye mtandao wa YouTube Ijumaa iliyopita.





Katika video ya muziki huo, mwanamuziki huyo wa rapa anateleza kwenye mlingoti kutoka peponi au mbinguni hadi jehanamu au motoni, akiwa amevaa viatu hivyo.





Taswira na hiyo na viatu ambavyo vimeandikwa andiko la Bibilia Luka 10:18 - "Akawaambia, 'Nilimuona shetani akianguka kama radi kutoka mbinguni'."





Kila kiatu kina soli maalum ya muundo wa kampuni ya Nike yenye sentimita za ujazo 60 za wino mwekundu na tone la damu ya binadamu, ambayo ilichangiwa na wanachama wa kampuni hiyo.





Kampuni ya Nike ambayo ni maarufu kwa viatu vya michezo imesema kuwa katika kesi yake iliyowasilishwa kwenye mahakama moja mjini New York, kuwa haiidhinishi au kuruhusu utengenezaji wa 'Viatu vya Shetani'.





Lil Nas X and MSCHF's Satan Shoes sold out in less than a minute on Monday
Maelezo ya picha,Viatu vya shetani vilivyozinduliwa na Rapa Lil Nas X kwa ushirikiano na kampuni ya MSCHF viliuzwa vyote chini ya dakika moja Jumatatu




Kampuni ya Nike inataka mahakama kusitisha kampuni ya MSCHF kuuza viatu hivyo na pia kuwazuia kutumia nembo yao ya muda mrefu maarufu kama 'Swoosh'.





"Kampuni ya MSCHF na viatu vyake vya shetani ambavyo havijaidhinishwa kuna uwezekano mkubwa kukasababisha mkanganyiko na dhana fulani na kutengeneza fikra mbaya kati ya bidhaa ya kampuni ya MSCHF na kampuni ya Nike," Kampuni hiyo ya utengenezaji viatu vya michezo imesema katika kesi yake iliyowasilisha.





"Kwanza, tayari kuna ushahidi wa kutosha unaoonesha mkanganyiko na dhana potofu sokoni, ikiwemo simu zinazotaka watu kususia bidhaa za kampuni ya Nike kufuatia uzinduzi wa viatu vya shetani vya kampuni ya MSCHF, ambavyo inaonekana kana kwamba kampuni ya Nike ndiyo ambayo imeidhinisha na kuruhusu utengenezaji wa bidhaa za hiyo."





Kesi iliyowasilishwa inarejelea ujumbe wa mtandao wa Twitter uliotumwa na mshawishi mkubwa wa viatu @Saint Ijumaa iliyopita, ambao ulianza kuarifu wateja wake kuhusu kuzinduliwa kwa viatu hivyo na kuvipa umaarufu zaidi kwa umma wikendi kwenye mtandao wa kijamii na hata vyombo vya habari vya Marekani.





Baadhi ya wenye msimamo mkali akiwemo gavana wa Dakota Kusini Kristi Noem, na wafuasi wengine wa kidini, wameshutumu viatu hivyo vyenye utata na kumkosoa rapa Lil Nas X na kamupuni ya MSCHF kwenye mtandao wa Twitter.





Hata hivyo, Lil Nas X alimjibu gavana huyo pamoja na viongozi wa kidini kwenye mtandao wa Twitter, na Jumatatu katika mtandao huo, kulikuwa na vibonzo vya mzaha kwenye wasifu wake baada ya kampuni ya Nike kusema kwamba imechukua hatua ya kisheria.


Share:

Philip Mpango apendekezwa kuwa Makamu wa Rais Tanzania


Rais Samia Suluhu Hassan ampendekeza Philip Isdory Mpango kuwa makamo wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Jina hilo liliwasilishwa bungeni asubuhi ya Jumanne na mpambe wa rais katika bahasha maalum.Baada ya kupokea Spika Job Ndugai alilitangazia bunge hilo jina hilo lililopendekezwa na Rais Samia.Mara baada ya tangazo hilo bunge lililipuka kwa shangwe.Bwana Mpango amekuwa waziri mwandamizi katika serikali ya hayati John Magufuli akihudumu kama waziri wa fedha.Kwa sasa, bunge la Tanzania linatarajiwa kupiga kura ili kuthibitisha uteuzi huo wa Mpango.Na kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, asilimia 50 ya wabunge wanatakiwa kuukubali uteuzi huo ili kuthibitishwa.

Kabla ya jina hilo kuwasilishwa bungeni hii leo, kwanza liliwasilishwa katika Kamati kuu ya chama tawala CCM na kuthibitishwa.

'Nimepigwa na butwaa'

Mara tu baada ya jina lake kusomwa Spika Ndugai alimpatia Mpango muda wa kujieleza ndani ya Bunge.

Mpango akaeleza kuwa hakujua chochote juu ya uteuzi huo na kwamba alipigwa na butwaa.

'...Hii ni heshima kubwa sana, sikuwahi kuota (kama nitaipata)...Mpaka Naibu Waziri wangu akiwa anajibu maswali asubuhi hapa, nilikuwa nafikiria majukumu yangu yanayonikabili ikiwemo mishahara ya wabunge ambayo baadhi imechelewa mpaka asubuhi hii. Nimepigwa na butwaa..."

Phillip Mpango ni nani?


Dkt.Mpango
Maelezo ya picha,Dkt. Phillip Mpango

Dkt. Philip Mpango amekua Waziri wa Fedha na Mipango katika Serikali ya Awamu ya Tano, ameteuliwa katika baraza la mwanzo la mawaziri la Rais John Magufuli.

Mwaka 2015 Alikua mbunge wa kuteuliwa.

Bwana Mpango ni mzaliwa wa Kigoma, baba yake ni marehemu Isidori Nzabhayanga Mpango, ambaye alizaliwa Kijiji cha Kasumo, Wilaya ya Kasulu.

Dkt. Mpango alizaliwa hapohapo Kasumo na ni kaka mdogo wa Askofu mstaafu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Tanganyika Magharibi - Kasulu mkoani Kigoma, Dk Gerard Mpango.

Dk Mpango ni mchumi mwenye shahada ya uzamivu ya uchumi.

Kuanzia miaka ya 1990 hadi 2000, alifanya kazi akiwa mhadhiri mwandamizi wa uchumi katika kitivo cha Biashara (sasa Shule ya Biashara) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Alikuwa akifundisha "Microeconomics", "Macroeconomics" (kwa mwaka wa pili) na "Public Finance" kwa mwaka wa tatu na kozi za uzamili. (Kwa tafsiri yangu, Uchumi mdogo, Uchumi mkubwa na masuala ya Fedha za umma.)

Amewahi kuwa Mchumi Mwandamizi wa Benki ya Dunia, Mkuu wa Kamati ya kumshauri Rais Jakaya Kikwete wakati huo kuhusu masuala ya uchumi, Katibu binafsi wa Rais anayeshughulikia masuala ya uchumi, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, kabla ya kuhamishiwa Tume ya Mipango, Ofisi ya Rais.

Nyadhifa hizi zote amezishika wakati wa utawala wa Kikwete.

JPM alipoingia madarakani alimteua kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na baada ya siku chache akateuliwa kuwa Waziri wa Fedha na Mipango.

Katika uchaguzi wa mwaka 2020 alishinda kiti Cha ubunge jimbo la Buhingwe.

Kisha kuteuliwa tena kuwa waziri wa fedha na Mipango.


Share:

Serikali yatangaza combination mpya tano



Serikali imetangaza kuanza kwa Combination mpya tano kwa ajili ya wanafunzi watakaoingia kidato cha tano mwaka 2021.

Lengo la kuongeza tahasusi hizo ni kuondoa changamoto ya ukosefu wa wataalam nchini ambayo imekuwepo kwa muda mrefu.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi, Seleman Jafo jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Combination hizo ni Fizikia, Hesabu na kompyuta (PMC); Kiswahili, French ,Chinese (KFC); Kiswahili, English, Chinese (KEC); Physical Education, Biology, Fine Art (PBF) na Physical Education, Geography, Economics (PGE).

“JAFO KAMA UMESHINDWA TUAMBIE, TAMISEMI MNACHUKUA FEDHA HAZIRUDI”- RAIS SAMIA AWASHA MOTO


Share:

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo March 30, 2021






Good Morning, kutoka Dar es salaam leo March 30, 2021,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za nyuma za Magazeti ya Tanzania.






































































Share:

PROF. OLE GABRIEL AMNASA ALIYEKUA AKIJARIBU KUKWEPA UTARATIBU WA KUSAFIRISHA MIFUGO


Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia idara zake za Uzalishaji na Masoko na ile ya Huduma za Mifugo kwa kushirikiana na jeshi la Polisi wamefanikiwa kumkamata Mfanyabiashara wa mifugo Bw. Joseph Bonifasi ambaye alikuwa anasafirisha Ng’ombe kuelekea mkoani Lindi kinyume na taratibu.

Tukio hilo limetokea Usiku wa Kuamkia leo (11.03.2021) katika kizuizi kilichopo eneo la Mbande jijini Dodoma ambapo Polisi walizuia gari iliyobeba ng’ombe hao na kumkamata mmiliki wake baada ya kuzitilia mashaka nyaraka zilizotumika kuwasafirishia.

“Baada ya kumkamata, alikataa kufuata taratibu zinazotakiwa na badala yake akampigia simu Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel na kwa kweli tunamshukuru sana Katibu Mkuu kwa sababu tofauti na alivyodhani mtuhumiwa wetu, yeye aliamuru ashikiliwe mpaka watendaji wa Wizara watakapofika hapo na kujiridhisha juu ya uhalali wa nyaraka hizo” Alisema mmoja wa Askari aliyekuwepo kwenye kizuizi hicho.

Muda mfupi baada ya kufika katika eneo la tukio, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Masoko Bw. Stephen Michael akiwa ameambatana na timu ya wataalam kutoka idara ya huduma za mifugo walikagua nyaraka hizo na kubaini dosari kadhaa ikiwemo kuisha kwa muda wa matumizi wa kibali kilichotumika kusafirishia mifugo hiyo.

“Lakini pia tumebaini kuwa kibali hiki kimetumika kusafirishia mifugo zaidi ya mara moja ambapo kimeonekana awali kilitumika kusafirishia mifugo mingine kutoka Tura kwenda Pugu kabla ya kutumika tena kusafirishia ng’ombe kwenda Mtwara kupitia Manyara, Dodoma, Morogoro na Pwani na mbaya zaidi taarifa za awali zimekatwa na kuandikwa nyingine kwa juu” Amesema Stephen.

Mbali na dosari zilizoonekana kwenye nyaraka za kusafirishia ng’ombe hao, Mfanyabiashara huyo pia amefanya kosa la kusafirisha ng’ombe wakubwa na watoto (ndama) kwa wakati mmoja kinyume na sheria ya haki za wanyama ya mwaka 2010 ambayo kipengele cha 8 (1) kinachohusu usafirishaji  ambacho kinaainisha kuwa mhusika ni lazima azingatie uzito,ukubwa na maumbo ya ng’ombe kabla ya kuwasafirisha kwa pamoja.

Kwa upande wake Mfanyabiashara huyo alikiri kufanya kosa la kutokuwa na nyaraka halali za kusafirishia ng’ombe hao ambapo pia alitoa wito kwa wafanyabiashara wenzake kutii sheria wakati wote wanapopaswa kufanya hivyo.

“Nitakuwa balozi mzuri kwa wenzangu na kuanzia sasa hata nikiona mfanyabiashara mwenzangu hajafuata taratibu za kusafirisha mifugo yake, ntakuwa wa kwanza kuripoti kwenye mamlaka husika” Amesema Bonifasi.

Hivi karibuni Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia sekta ya Mifugo iliunda kikosi kazi maalum kwa ajili ya kufanya doria ya kudhibiti utoroshwaji wa mifugo mipakani na kwenye vizuizi mbalimbali zoezi ambalo tayari limeshaonekana kuanza kuzaa matunda.










Share:

HABARI MAGAZETI YA LEO MACHI 12,2021


Pata vichwa vya habari kwenye magazeti ya leo




















































































Share: